Pages

Monday, May 19, 2014

KLABU YA DARAJA LA KWANZA YAMSAJILI RAIS WA BOLIVIA KATIKA NAFASI YA KIUNGO


Timu moja ya soka ya wachezaji wa kulipwa ya nchini Bolivia imemsajili rais Evo Morales kama mchezaji wao kiungo atakayeichezea timu hiyo katika msimu ujao.

Morales mwenye miaka 54 ni shabiki mkubwa wa soka, na msimu ujao ataichezea klabu ya Sport Boys, yenye maskani yake kusini-mashariki mwa mkoa wa Santa Cruz.

Timu hiyo ya daraja la kwanza imesema rais Morales atakuwa anacheza soka kwa dakika 20 tu katika mechi moja lakini si kila mchezo kutokana na ratiba yake ya majukumu ya taifa.

Rais Morales atakuwa atalipwa na kabu hiyo mshahara wa kiasi cha dola 214.

No comments:

Post a Comment