Baada
ya kutolewa kwa Manchester City na Arsenal katikati ya wiki iliyopita,
Chelsea imejikatia tiketi ya kuingia Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa
kwa kuifunga mabao
2-0 timu hiyo ya Uturuki. Kwa ushindi huo Chelsea imepita kwa jumla ya magoli 3-1 baada ya suluhu ya 1-1 wiki mbili zilizopita nchini Uturuki.

2-0 timu hiyo ya Uturuki. Kwa ushindi huo Chelsea imepita kwa jumla ya magoli 3-1 baada ya suluhu ya 1-1 wiki mbili zilizopita nchini Uturuki.
Mabao
ya Chelsea yamefungwa Samuel Eto'o dakika ya nne na Gary
Cahil dakika ya 43.

Wakati huo huo klabu ya Real Madrid yatinga Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kufuatia ushindi wa mabao
3-1 usiku huu Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid ambao unawafanya
wasonge mbele kwa ushindi wa jumla wa mabao 9-2 dhidi ya Schalke ya
Ujerumani.
Mabao
yaliyoipeleka Madrid Nane Bora ya Ligi ya Mabingwa yamefungwa na
Cristiano Ronaldo mawili dakika za 21 na 74 akifikisha mabao 41 msimu
huu, na lingine limefungwa na Alvaro Morata dakika ya 75.
Madrid ilishinda 6-1 katika mchezo wa kwanza ugenini, hivyo imesonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 9-2.
No comments:
Post a Comment