Pages

Wednesday, April 9, 2014

MATOKEO: CHELSEA WALE NUSU FAINALI LIGI YA MABINGWA ULAYA



Bao la dakika ya 88 la Demba Ba limeivusha Chelsea hadi Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa faida ya bao la ugenini baada ya sare ya jumla 3-3, ikishinda 2-0 Uwanja wa Stamford Bridge, London.
Andre Schurrle alitangulia kuifungia Chelsea dakika ya 32, akimalizia pasi ya David Luiz hadi mapumziko wenyeji walikuwa mbele kwa bao 1-0.
Waleteeeeeeeeee
Jose Mourinho alikuwa mwenye furaha kubwa leo baada ya bao Ba
Kocha Jose Mourinho ambaye timu yake ilifungwa 3-1 katika mchezo wa kwanza mjini Paris, Ufaransa alipagawa kwa furaha baada ya bao la Ba akaenda kushangilia na wachezaji wake kwenye kibendera.

No comments:

Post a Comment