Akiwa kaambatana na viongozi wenzake wa tume Mh
Warioba alitumia zaidi ya saa nne kulihutumbia bunge hilo ambapo
amesema kutokana maoni waliyokusanya kutoka kwa wananchi
wanaapendekeza kuwepo na serikali tatu.
Hotuba hiyo ambayo mara kwa mara ilikuwa
ikikatishwa kwa shangwe makofi ya hapa na pale pia iligusia changamoto
kadhaa zilizopo katika muungano.
Wakati wa uwasilishwaji wa rasimu hiyo mwenyekiti
huyo ambaye amewahi kuwa waziri mkuu wa jamhuri ya muungaano wa
Tanzania katika hotuba yake kwa nyakati tofauti tofauti mwenyekiti wa
bunge maalum la katiba na makamu wake walikuwa wanalazimika kuwatuliza
wajumbe ili kuleta usikivu.
Awali itakumbukwa kuwa rasimu hiyo ilipaswa
kuwasilishwa bungeni mapema jumatatu lakini zoezi hilo lilikwama kwa
kile kilichoelezwa kuwa kanuni zili kiukwa na hapa Mh Sitta anatoa
ufafanuzi ya makubaliano yaliyofikiwa.
Katika hatua nyingine bunge lililazimika kupumzika
kwa muda baada ya Mh Warioba kukiomba kiti apewe muda kidogo wa
kupumzika baada ya kusimama kwa takribani saa moja.
No comments: