Wananchi wakiangalia daladala iliyopata ajali juzi usiku katika eneo la Kijiji cha Mkupuka, wilayani Rufiji, Mkoa wa Pwani.
Siku moja baada ya ajali kuua watu 12 wilayani Same, ajali nyingine mbili mbaya zilizohusisha magari matano zimetokea katika eneo moja wilayani Rufiji na kuua watu 22, akiwamo kondakta wa gari aina ya Toyota Hiace ambaye kichwa chake kimetenganishwa na kiwiliwili.
Ajali hizo zilizopishana kwa dakika chache zilitokea juzi saa 1:00 jioni katika Kitongoji cha Mkupuka, Kata ya Kibiti na zilisababisha vifo vingi kutokana na watu 14 waliojeruhiwa katika ajali ya kwanza iliyoua watu saba, kukanyagwa na gari jingine wakati wakisubiri kupandishwa kwenye gari aina ya Toyota Land Cruiser la Idara ya Maliasili ili kupelekwa hospitali.
Habari kutoka Kituo cha Afya cha Ikwiriri zinaeleza kuwa miili ya watu wawili ilitenganishwa kichwa na kiwiliwili, maiti tano zilikuwa na vichwa vilivyopasuka na maiti nyingine zilikuwa zimekatikakatika mifupa.
Siku moja baada ya ajali kuua watu 12 wilayani Same, ajali nyingine mbili mbaya zilizohusisha magari matano zimetokea katika eneo moja wilayani Rufiji na kuua watu 22, akiwamo kondakta wa gari aina ya Toyota Hiace ambaye kichwa chake kimetenganishwa na kiwiliwili.
Ajali hizo zilizopishana kwa dakika chache zilitokea juzi saa 1:00 jioni katika Kitongoji cha Mkupuka, Kata ya Kibiti na zilisababisha vifo vingi kutokana na watu 14 waliojeruhiwa katika ajali ya kwanza iliyoua watu saba, kukanyagwa na gari jingine wakati wakisubiri kupandishwa kwenye gari aina ya Toyota Land Cruiser la Idara ya Maliasili ili kupelekwa hospitali.
Habari kutoka Kituo cha Afya cha Ikwiriri zinaeleza kuwa miili ya watu wawili ilitenganishwa kichwa na kiwiliwili, maiti tano zilikuwa na vichwa vilivyopasuka na maiti nyingine zilikuwa zimekatikakatika mifupa.
Picha na Amini Yasini
No comments: