
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Bw. Leonard Thadeo akisalimiana na
wachezaji wa Timu ya Shirika la Taifa la Bima (NIC) Uganda wakati wa
fainali ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki kwa mchezo wa Netiboli, ambayo
walicheza na JKT – Mbweni ya ya Tanzania
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Bw. Leonard Thadeo akimkabidhi Kombe la mshindi wa kwanza wa mashindano ya netiboli Klabu Bingwa Afrika Mashariki nahodha wa Timu ya NIC Uganda ,Obua Desire, baada ya kuifunga timu ya JKT Mbweni ya Tanzania magoli 47 – 30.

Wachezaji wa timu ya NIC Uganda wakifurahia ushindi uliopelekea kutetea ubingwa wao jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Chama cha mpira wa Netiboli Tanzania (Chaneta) Bi. Anna Kibira 9kusoto) akikabidhiwa majukumu ya Shirikisho la vyama vya mpira wa netiboli Afrika Mashariki (EANA) na Rais wa Shirikisho hilo Bi.Mildred Ajiemba Wanyama juzi jijini Dar es Salaam. Tanzania imekabidhiwa kuongoza sekretariati ya shirikisho hilo kutoka nchi ya Kenya.
Picha na Frank Shija, Afisa Mawasiliano Serikalini.
No comments: