
Afisa habari kitengo cha habari Umoja wa mataifa nchini
Tanzania(UNIC) Bi. Usia Nkhoma Ledama akizungumza katika viwanja vya
Mazingira Senta mjini Shinyanga kwenye warsha ya siku moja
iliyokutanisha shule 10 za sekondari, vyuo na walimu kutoka katika shule na vyuo hivyo vilivyopo katika manispaa ya Shinyanga, ambapo alisema Umoja wa Mataifa(UN) unalipa suala la elimu kipaumbele sana kwa wanafunzi hivyo kuwataka wanafunzi kuwa na malengo katika maisha yao kwa kusoma kwa bidii,kuepuka vishawishi vinavyopelekea kupata ujauzito wakiwa wanafunzi tena chini ya umri wa miaka 18.
Afisa habari huyo pia aLItumia fursa hiyo kuwatahadharisha wanafunzi wa kike kuepuka ngono kwani kwa mujibu wa utafiti wao takwimu zinaonesha kuwa vijana wa kike wenye umri wa miaka 15-19 wana uhusiano wa kingono na wanaume wanaowazidi miaka juu zaidi ya umri wao hivyo kuwepo kwa hatari ya kuambukizwa VVU na Mimba za utotoni.Kushoto ni Mwenyekiti wa taasisi ya Umoja wa Mataifa Tanzania (UNA) tawi la Shinyanga bwana Ezra Manjerenga.

No comments: