MAANDALIZI ya ujenzi wa kijiji cha michezo kitakachojulikana kama
Jakaya Kikwete Sports Village yanaendelea vizuri, ambako tayari Ikulu,
Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na Wizara ya Michezo wametoa baraka
kijengwe mjini Dodoma.
Akizungumza na Tanzania Daima, Mratibu wa ujenzi wa kituo hicho, Wilhelm Gidabuday, alisema ujenzi wa kituo hicho kikubwa na cha kwanza nchini, tayari maandalizi yake yameshafikia pazuri na Ikulu ya Tanzania kupitia ofisi ya Katibu wa Rais, imeshawapa baraka ya kutumia jina la Rais katika kituo hicho.
Gidabuday alisema, wiki iliyopita walikutana na Katibu wa Rais, ambako waliwasilisha maombi yao na kukubaliwa na kwamba, kuanzia sasa kituo hicho ambacho ujenzi wake utasaidia kuinua vipaji vya michezo yote hapa nchini, kitafahamika kama kituo cha michezo cha Jakaya Kikwete (Jakaya Kikwete Sports Village).
Akizungumza na Tanzania Daima, Mratibu wa ujenzi wa kituo hicho, Wilhelm Gidabuday, alisema ujenzi wa kituo hicho kikubwa na cha kwanza nchini, tayari maandalizi yake yameshafikia pazuri na Ikulu ya Tanzania kupitia ofisi ya Katibu wa Rais, imeshawapa baraka ya kutumia jina la Rais katika kituo hicho.
Gidabuday alisema, wiki iliyopita walikutana na Katibu wa Rais, ambako waliwasilisha maombi yao na kukubaliwa na kwamba, kuanzia sasa kituo hicho ambacho ujenzi wake utasaidia kuinua vipaji vya michezo yote hapa nchini, kitafahamika kama kituo cha michezo cha Jakaya Kikwete (Jakaya Kikwete Sports Village).

“Nidokeze tu kuwa mipango yote inakwenda sawa tumeshafikisha ujumbe wetu Ikulu na imekubalika, awali tulipanga kituo chetu tukiite John Steven Akhwari Sports Village lakini baada ya kukaa na Mzee Akhwari, kwa pamoja tuliridhia kituo hiki kitumike kama sehemu ya kumpa heshima Rais wetu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete hivyo kitafahamika kama Jakaya Kikwete Sports Village” alisema Gidabuday.

No comments: