Jumamosi
ya tarehe 29 March 2014, watanzania waishio na wasomao Malaysia
walikutana katika Ubalozi wa Tanzania na kuunda Jumuiya mpya ya
Watanzania wanaoishi South East Asia.

Uongozi wa Wana Jumuiya hiyo ambao kwa kuanzia ni Watanzania waliopo Malaysia wakiwa na Balozi Mpya wa Tanzania,Dr. Aziz Ponary Mlima (katikati) na maafisa wa Ubalozi. Viongozi waliochaguliwa ni Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Katibu Mkuu, Waziri wa Fedha, Waziri wa Elimu, Waziri wa Jamiii, Utamaduni na Starehe ikiwa pamoja na Wadhamini wawili.

Watanzania wote kwa pamoja na wafanyakazi wa Ubalozi na Balozi Mpya wa Tanzania nchini Malaysia.
Jumuiya hiyo ilianzishwa Mwishoni mwa wiki,ambayo inajulikana kama " Tanzanian Diaspora in South East Asia" ambayo itakuwa inawashirikisha Watanzania wote katika nchi za Malaysia, Indonesia, Thailand, Philippines, Brunei, Laos na Cambodia.
Picha zaidi zinaweza kuonekana kwenye Ukurasa wa Facebook
https://m.facebook.com/pages/Tanzania-Diaspora-South-East-Asia/672703012775883?id=672703012775883&_rdr
Watanzania kutoka maeneo hayo wanaombwa kujiunga ili tuweze kutambuana na itakapokuwa lazima kusaidiana.
Kwa niaba ya Tanzanian Diaspora South East Asia.
Picha zaidi zinaweza kuonekana kwenye Ukurasa wa Facebook
https://m.facebook.com/pages/Tanzania-Diaspora-South-East-Asia/672703012775883?id=672703012775883&_rdr
Watanzania kutoka maeneo hayo wanaombwa kujiunga ili tuweze kutambuana na itakapokuwa lazima kusaidiana.
Kwa niaba ya Tanzanian Diaspora South East Asia.
No comments: