Siku
mbili baada ya kumalizika kwa mashindano ya kutafuta klabu bingwa wa
taifa wa mpira wa kikapu nchini Tanzania, baadhi ya makocha waliokuwa
wanazinoa timu zao katika michuano hiyo pamoja na wachezaji
wamefurahishwa na juhudi za Uongozi wa shirikisho ulioingia madarakani
hivi karibuni kwa kuongeza idadi ya timu zilizoshiriki michuano hiyo.
Makocha
Joseph wa savio na Bakari wa timu ya Bandari ya jijini Tanga pamoja na
Nahodha wa Savio, Roman Anania wamesema michuano ya mwaka huu imekuwa na
mafanikio makubwa kutokana na ushiriki wa timu nyingi katika michuano
hiyo. Wakati huo huo, Katibu mkuu wa Shirikisho la Mpira wa kikapu
Tanzania TBF Salehe Zonga amesema wapo mbioni kuanza mchakato wa
kutafuta vijana watakaoshiriki katika michuano mbalimbali ya kimataifa
yanayotarajiwa kuanza hivi karibuni jijini Kampala nchini Uganda.
No comments: