ads

Slider[Style1]

Style2

Style3[OneLeft]

Style3[OneRight]

Style4

Style5

 Mkuu wa Mahusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Bw. Stephen Kilindo (kulia) na Afisa Uhusiano wa Kampuni hiyo, Bi. Doris Malulu wakimuongoza Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Elias Kwesi (wa pili kushoto) kwenda kuzindua rasmi mradi wa maji katika Zahanati ya Mvuti, Kata ya Msongola, Wilayani Ilala, Dar es Salaam uliojengwa na TBL. 
 Kwesi (mwenye suti), akimshika mkono wa pongezi Afisa Uhusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Bi. Doris Malulu (wa pili kulia) wakati wakielekea kuzindua mradi wa maji katika zahanati ya Mvuti, iliyoko Kata ya Msongola, Manispaa ya Ilala, Dar es Salaam ulichojengwa na TBL. Kulia ni Mkuu wa mahusiano na sheria wa Kampuni hiyo Bw. Stephen Kilindo.
 Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Elias Kwesi (mwenye suti), akikata utepe kuzindua rasmi mradi wa maji katika Zahanati ya Mvuti, Kata ya Msongola, Wilayani Ilala, Dar es Salaam uliojengwa na Kampuni Bia Tanzania (TBL). Wa pili kulia ni Mkuu wa mahusiano na sheria wa Kampuni hiyo Bw. Stephen Kilindo Diwani wa Kata hiyo Bi. Angelina Malembeka na Ofisa Mauzo wa TBL Ilala Bw. Godrack Kalebi.

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Elias Kwesi (mwenye suti kulia), akiondoa kitambaa kuzindua mradi wa maji katika Zahanati ya Mvuti, Kata ya Msongola Manispaa ya Ilala, Dar es Salaam uliojengwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), anayemsaidia ni Ofisa Mauzo wa TBL Ilala Bw. Godrack Kalebi. Wanaoshudia ni Mkuu wa Mahusiano wa TBL, Bw. Stephen Kilindo na Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Dkt. Asenga Severin.  
 Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Elias Kwesi (mwenye suti), akijaribu kufungua koki ya bomba la maji, baada ya kuzindua mradi wa maji katika Zahanati ya Mvuti, iliyoko Kata ya Msongola, Manispaa ya Ilala, Dar es Salaam kilichojengwa na Kampuni Bia Tanzania (TBL). Wa pili kulia ni Mkuu wa mahusiano na sheria wa Kampuni hiyo, Bw. Stephen Kilindo, Ofisa Mauzo wa TBL,  Ilala, Bw. Godrack Kalebi na Ofisa Uhusiano wa kampuni hiyo, Bi. Doris Malulu.
 Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Elias Kwesi (mwenye suti), akisaidia kumtwisha ndoo ya maji mkazi wa kijiji cha Mvuti, Bi. Aghata Senga, baada ya kuzindua mradi wa maji katika Zahanati ya Mvuti, iliyoko Kata ya Msongola Manispaa ya Ilala, Dar es Salaam uliojengwa na Kampuni Bia Tanzania (TBL). kulia ni Mkuu wa Mahusiano na sheria wa TBL, Bw. Stephen Kilindo Ofisa Mauzo wa TBL kanda ya Ilala Bw. Godrack Kalebi (wa pili kulia) na Diwani wa Kata hiyo Bi. Angelina Malembeka (mwenye kilemba kushoto).

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment


Top