Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea cheti maalum cha ulezi wa heshima
wa Chama cha wenza wa mabalozi wa nchi za Afrika walioko nchini Ubelgiji
(Honory Patronese of the Association of the Spouses of African
Ambassadors in Belgium) kutoka kwa Mke wa Balozi wa Cameroon nchini
Ubelgiji Mama Christiane Eloundov de Evina wakati wa chakula cha mchana
walichowaandalia wake wa Marais wa Afrika jijini Brussels tarehe
2.4.2014
Mke
wa Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji Mama Adelaida Kamala akimkabidhi
Cheti Maalum cha ulezi wa heshima cha wenza wa mabalozi wa Afrika
walioko Ubelgiji, Mke wa Rais wa Cameroon Mama Chantal Biya wakati wa
chakula cha mchana walichowaandalia wageni hao kwenye hoteli ya
Sheraton.
Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete amepewa cheti na Umoja wa wake wa Mabalozi
wa Afrika waishio katika nchi za Jumuia ya Ulaya kwa kutambua na
kuthamini mchango wake na kazi anazozifanya za kuwasaidia wanawake,
wasichana na watoto wa Tanzania.
Cheti
hicho amekabidhiwa jana katika hafla fupi ya chakula cha mchana
kilichoandaliwa na wake hao wa mabalozi katika ukumbi wa mikutano uliopo
Hoteli ya Sheraton mjini Brussels.
Mama
Kikwete ni mmoja kati ya wake wa Marais wa tano wa Afrika
waliokabidhiwa vyeti hivyo vya heshima kutokana na kazi zao
wanazozifanya za kuisaidia jamii na kuhakikisha kuwa inapata mahitaji ya
muhimu kama huduma ya afya na elimu.
Akiongea
kabla ya kuwakabidhi wake hao wa marais vyeti hivyo Mke wa Balozi wa
Equatorial Guinea ambaye pia ni rais wa umoja huo Mama Mangue de Nvono
Nca alisema nia ya kuanzishwa kwa umoja wao ni kulitambulisha bara la
Afrika ambalo linajulikana kuwa na changamoto za njaa, magonjwa,
kutokuwa na haki na usalama wa kutosha katika nchi za Ulaya.
No comments: