ads

Slider[Style1]

Style2

Style3[OneLeft]

Style3[OneRight]

Style4

Style5

Cristiano Ronaldo jana alifunga bao tamu sana na kuinusuru Real Madrid kupoteza mechi.

Valencia ilionekana kubeba pointi zote tatu Uwanja wa Santiago Bernabeu, lakini mshindi huyo wa Ballon d'Or aliinusuru timu yake tena, alipounganisha krosi ya Angel di Maria kwa utaalamu wa hali ya juu. 
Mathieu alianza kuifungia Valencia dakika ya 44, lakini Sergio Ramos akaisawazishia Real Madrid dakika ya 59na Parejo akawafungia wageni bao la pili, kabla ya Ronaldo kufunga lake la 50 msimu huu. 
Licha ya Atletico kufungwa 2-0 na Levante jana, bado ipo kileleni mwa La Liga kwa pointi zake 88 za mechi 36, ikifuatiwa na Barcelona pointi 85 mechi 36 wakati Real sasa ni ya tatu kwa pointi zake 83 za mechi 35. 
 Nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo amefunga bonge la bao jana katika sare ya 2-2 na Valencia
 Ronaldo (katikati) akimtoka mchezaji wa Valencia, Juan Bernat (kushoto)

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment


Top