ads

Slider[Style1]

Style2

Style3[OneLeft]

Style3[OneRight]

Style4

Style5


Ilipoishia Maria: " mpenzi jiandae kesho ntakufuata Gengeni kwako tuongozane kuna vitu naenda kukununulia"

Endelea
Johnson alifurahi sana kusikia vile japo hakujua anaenda kununuliwa vitu gani akaona kweli yale maneno ya Mzee Joseph yamefanya kazi, alivyomaliza kuongea na Maria akakata simu akalala zake huku akitamani kukuche haraka aonane na Maria akaone hivyo vitu anavyoenda kununuliwa.
Asubuhi kama kawaida aliwahi kuamka akajiandaa akaenda gengeni kwake kufungua, alivyomaliza kupanga kila kitu akachukua gazeti akawa anasoma huku anamsubiri mpenzi wake Maria kwa hamu.
Wakati anasoma gazeti pale akamuona mzee Joseph anamfuata pale gengeni kwake alifurahi sana sababu muda mwingi alikuwa anapenda kukaa na Mzee Joseph alikuwa anampa sana maujanja ya kuishi pale mjini alikuwa anamfundisha vitu vingi sana ambavyo alikuwa havijui.
Mzee Joseph alifika pale wakasalimiana lakini mzee Joseph akamuona kama Johnson ana furaha sana ile siku. Akaamua kumuuliza, vipi kijana wangu mbona leo unaonekana umefuraha sana?
Johnson: "yani we acha tu mzee wangu kweli nimekukubali nimeshaanza kuona maneno yako yanafanya kazi kidogo kidogo"
Mzee Joseph akacheka akamuuliza, kwani kuna nini kijana mbona sijakuelewa?

Johnson: "jana usiku nilimpigia simu mpenzi wangu Maria nikawa namuuliza habari za nyumbani kwao kama amefika salama, akaniambia kafika salama hakuna tatizo na ameniambia leo ananifuata hapa tunaongozana kuna vitu anaenda kuninunulia zawadi"
Mzee Joseph: "hayo ndio mambo sasa kijana si unaona sasa ujanja niliokupa sio wewe una mrembo kwao wana pesa vile upo naye siku nyingi unashindwa kutajirika hadi leo unahangaika kuuza genge"
Johnson akacheka: "mimi ndio maana nakukubali mzee yani hujawahi kuniambia kitu halafu kikaenda tofauti ngoja tu tumsubiri mrembo tujue zawadi anazoenda kuninunulia"
Mzee Joseph akamtania Johnson: "sasa sio mpenzi wako anaenda kukununulia mazawadi kibao halafu mimi unanisahau wakati mimi ndio nimekusanua ukifanya hivyo lazima nikuharibie kwa Maria wako aache kukupa pesa"
Johnson alicheka sana kusikia vile: "we mzee huwezi kuniharibia kwa Maria nimetoka nae mbali sana lakini siwezi kukusahau wewe ni mzee wangu lazima na wewe nikuletee zawadi nakukubali sana"
Wakati Mzee Joseph na Johnson wanapiga stori pale gengeni simu ya Johson ikawa inaita kuangalia alikuwa ni Maria, akapokea haraka wakasalimiana.

Maria: "mpenzi wangu nikukute umejiandaa nipo kwenye bajaji nakuja hapo kukufuata tuondoke" Johnson: "sawa mpenzi wangu ngoja nianze kufunga genge langu haraka haraka"
Maria alivyokata tu simu Johnson akamwambia mzee Joseph "mzee Maria kanipigia simu yupo njiani anakuja ngoja nifunge hapa akifika tu tuondoke"
Mzee: "sawa kijana kale maisha na mrembo na umuambie akununulie vitu vya maana sio unafika huku unanunuliwa zawadi za kitoto nawe unakubali, utakuwa hukanyagi hapa"
Johnson: "sawa mzee nimekusoma siwezi kukubali zawadi za kitoto kwani mimi mtoto"

Johnson alimaliza kufunga genge lake akawa anamsubiri Maria afike waondoke

Inaendelea………………….

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Post a Comment


Top